Searching...
Sunday, February 13, 2011

Misri washerekea kuondoka kwa Mubarak

Maelfu ya wananchi wa Misri bado wametapakaa katika eneo la wazi la Tahrir mjini Cairo, siku moja baada ya kujiuzulu kwa Rais Hosni Mubarak.
Cairo
Waandamanaji wamekesha Tahrir
Katika hali ya sherehe, watu wameanza kusafisha eneo hilo la wazi, huku wanajeshi wakiondoa vizuizi, ingawa vifaru bado vimesalia.
Baada ya miaka 30 madarakani, Bw Mubarak alilazimishwa kuondoka madarakani kufuatia siku 18 za maandamano ya kupinga serikali.
Cairo
Sherehe baada ya Mubaraka kutangaza kuondoka
Nchi sasa iko mikononi mwa jeshi.
Rais wa Marekani Barak Obama ameita nchi ya Misri kuwa yenye kuhamasisha, lakini amesema lazima nchi hiyo ielekee katika utawala wa kiraia na wa kidemokrasia.
Rais huyo amemtuma Adm Mike Mullen, mwenyekiti wa wakuu wa jeshi la Marekani, kwenda Jordan na Israel kujadili hali ya mabadiliko ya Misri.
Cairo
Waandamanaji Tahrir
Muda mfupi kabla ya tangazo la kujiuzulu, Bw Mubarak aliondoka mjini Cairo kuelekea mji wa Sharm el-Sheikh uliopo kwenye pwani ya bahari ya Sham, ambapo ana makazi yake mengine.
Mandamano ya kupinga serikali yaliyoanza Januari 25, yalichochewa na kuenea kwa hali ya mashaka nchini Misri, kutokana na ukosefu wa ajira, umasikini na ufisa

0 comments:

WELCOME URARY95 SPORTS NEWS BLOG | ADVERTISE YOUR BUSINESS HERE AT A CHEAP PRICE MORE INFORMATION CONTACT US: 0654315901 | Email: urary95@yahoo.com | KARIBU URARY95 SPORTS NEWS BLOG | TANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA GHARAMA NAFUU KWA MAELEZO ZAIDI WASILIANA NASI: 0654315901 | Barua Pepe: urary95@yahoo.com
 
Back to top!