Baada ya wiki mbili za maandamano ya kuipinga serikali nchini Misri, makamu wa Rais Omar Suleiman ameanza mazungumzo na makundi ya upinzani.

Waandamanaji wakimiminika kwenye uwanja wa Tahrir, Cairo
Taarifa zinasema tayari makubaliano yamefanyika ya kuunda kamati ya kuchunguza mabadiliko yanayotakiwa kufanyika katika katiba ya nchi hiyo.
Kundi la Muslim Brotherhood ambalo bado limepigwa marufuku nchini Misri lilikuwa limesema linasubiri kuona ikiwa serikali iko tayari kufanya mabadiliko ya kisiasa mara moja.

Kundi la Muslim Brotherhood
Hii ni mara ya kwanza kwa serikali ya Misri kufanya mazungumzo na kundi hilo la Muslim Brotherhood lililopigwa marufuku.
Makundi ya upinzani yanataka Bw Mubarak kujiuzulu mara moja lakini amesema kuondoka kwake kwa dharura kutaleta vurugu.
Aidha, amesema hatagombea kiti cha urais katika uchaguzi utakaofanyika mwezi Septemba.
Wakati huo huo, benki zilizokuwa zimefungwa kwa zaidi ya juma moja zimefunguliwa huku kukiwa na wasi wasi kwamba watu wengi watatoa pesa zao kutoka benki kufikia kiwango kikubwa mno.

Raia wantoa pesa kutoka benki
Halaiki ya watu wamekuwa wakiandamana katika mitaa ya Cairo na miji mingine majuma mawili yaliyopita wakitaka mabadiliko katika mfumo wa demokrasia.
Kabla ya mazungumzo msemaji wa Muslim Brotherhood, Mahmoud Azzat, alisema wakuu wameanza kukubali shuruti zao.
Lakini maandamano yanaendelea leo katika medani Tahrir mjini Cairo.


0 comments:
Post a Comment