Waziri wa Ustawishaji wa Viwanda nchini Kenya, Henry Kosgey, ambaye alikuwa amepangiwa kufikishwa maakamani na maafisa wa taasisi ya kupambana na rushwa, amejiuzulu wadhifa wake.

Nairobi
Bwana Kosgey ni mwenyekiti wa chama cha ODM cha Waziri Mkuu Raila Odinga na pia ni mmoja wa Wakenya sita wanaoshutumiwa na Mahakama ya Kimataifa ya uhalifu, ICC, kupanga machafuko baada ya uchaguzi miaka mitatu iliyopita.
Chama cha ODM hata hivyo kimesema kitaendelea kumuunga mkono Kosgey.


0 comments:
Post a Comment