Watu saba, wakiwemo watoto, wamejeruhiwa katika mlipuko wa bomu katika mji mkuu wa Rwanda, Kigali.

Ramani ya Rwanda
Msemaji wa polisi alieleza majeruhi walipelekwa hospitalini na kutibiwa kwa majeraha madogo madogo waliyoyapata.
Alitoa wito kwa watu walio na silaha kinyume na sheria kuzisalimisha katika vituo vya polisi.
Waandishi wa habari wanasema mfuluflizo wa milipuko ya mabomu nchini Rwanda, mwaka jana ilisababisha vifo vya watu watatu na kuwajeruhi wengine kadha.


0 comments:
Post a Comment