Searching...
Tuesday, January 4, 2011

Mlipuko wa bomu wajeruhi saba Kigali

Watu saba, wakiwemo watoto, wamejeruhiwa katika mlipuko wa bomu katika mji mkuu wa Rwanda, Kigali.
Ramani ya Rwanda
Ramani ya Rwanda
Polisi wamesema tukio hilo lilitokea siku ya Jumapili, wakati mtoto mwenye umri wa miaka 11, alipoliokota bomu hilo kando ya barabara.
Msemaji wa polisi alieleza majeruhi walipelekwa hospitalini na kutibiwa kwa majeraha madogo madogo waliyoyapata.
Alitoa wito kwa watu walio na silaha kinyume na sheria kuzisalimisha katika vituo vya polisi.
Waandishi wa habari wanasema mfuluflizo wa milipuko ya mabomu nchini Rwanda, mwaka jana ilisababisha vifo vya watu watatu na kuwajeruhi wengine kadha.

0 comments:

WELCOME URARY95 SPORTS NEWS BLOG | ADVERTISE YOUR BUSINESS HERE AT A CHEAP PRICE MORE INFORMATION CONTACT US: 0654315901 | Email: urary95@yahoo.com | KARIBU URARY95 SPORTS NEWS BLOG | TANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA GHARAMA NAFUU KWA MAELEZO ZAIDI WASILIANA NASI: 0654315901 | Barua Pepe: urary95@yahoo.com
 
Back to top!