Searching...
Monday, January 3, 2011

MAJONZI NA HUZUNI HYDERABAD,INDIA

Marehemu shakir Hamdoun Al-marhubi
Marehemu alikuwa ni mwanafunzi wa chuo kikuu cha Osmania alikuwa  akisoma kozi ya BCA katika chuo hicho kilichoko hapa hyderabad,mwili wa marehemu ulikutwa nyumbani kwake alipokuwa anaishi taarifa za kifo chake cha nini kimemuondoa marehemu hazijajulikana hadi sasa inasadikiwa alifariki siku zisizopungua tano nyuma mwili wake ulikutwa ndani ukiwa umevimba tena ni baada ya kutoa harufu nje ndio majirani wakashituka,mwili wa marehemu umepelekwa Gandhi hospital kwa uchunguzi zaidi

Marehemu mwenye shati nyekundu akiwa na rafiki zake hapa hyderabad
Marehemu wa pili kutoka kulia enzi za uhai wake hapa akiwa uwanjani masab tank
wa tatu kutoka kushoto kwako ..akiwa kwenye sherehe ya mahafali ya wa wanafunzi tsah
Mkiti mstahafu TSAH Bw,Nkya akiwa mazishini sainikpuri
Mkiti wa kamati ya starehe TSAH mstahafu mwenye aliyevaa shati nyekundu alikuwepo kwenye mazishi na ndie aliyetayarisha hizi picha ...
Mwenye fulana nyeusi ktkt Mr Abdul Aziz ndie alikuwa mtu wake wa karibu sana
kwenye mazishi sainikpuri
Aliyesimama ni sheikh Mohammed Best akitoa mawaidha kwenye mazishi
hii ndio nyumba mazishi yalipofanyikia
kwa kweli wanafunzi walishikwa na simanzi sana
walijitokeza wanafunzi wengi sana ,kuonesha kuwa bado wanampenda ndugu yao
TULIKUPENDA SANA NDUGU YETU LAKINI MWENYEZI MUNGU AMEKUPENDA ZAIDI
tunamuomba Mwenyezi mungu ailaze roho ya marehemu mahali pepa peponi
AMIN

0 comments:

WELCOME URARY95 SPORTS NEWS BLOG | ADVERTISE YOUR BUSINESS HERE AT A CHEAP PRICE MORE INFORMATION CONTACT US: 0654315901 | Email: urary95@yahoo.com | KARIBU URARY95 SPORTS NEWS BLOG | TANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA GHARAMA NAFUU KWA MAELEZO ZAIDI WASILIANA NASI: 0654315901 | Barua Pepe: urary95@yahoo.com
 
Back to top!