Jopo la Umoja wa Mataifa lililotwikwa jukumu la kuangalia zoezi la kura ya maoni ya kuamua hatma ya eneo la Sudan Kusini limeelezea kuridhishwa kwake na jinsi zoezi hilo lilivyoendeshwa likisema kuwa zoezi hilo lilikuwa na mpangilio mzuri na kuwawesesha wenyeji kuelezea hisia zao bila vizuizi.
Jopo hilo liliwapongeza watu wa Sudan kwa kuhakikisha kuwa kura hiyo iliendeshwa wakati uliowekwa na kwa amani na kuipa pongezi tume iliyosimamia kura hiyo kwa kufanikisha kura hiyo.
0 comments:
Post a Comment