Searching...
Tuesday, January 11, 2011

Huku upigaji kura ukiendelea ghasia zalipuka Abyei-Sudan


 Abyei
Askari wa Sudan Kusini akisindikiza msafara wa watu wanaorudi kutoka kaskazini kuelekea Abyei.
Maafisa wa Sudan wanasema watu wapatao 36 wameuwawa katika siku 3 za mapigano makali katika wilaya iliyo na mzozo wa Abyei huku wapiga kura wakiendelea kufurika katika vituo vya kupigia kura katika tukio la kihistoria la kura ya maoni ya Sudan Kusini.
Viongozi wa makabila ya kaskazini ya Misseriya na wale wa kusini Ngok Dinka waliendelea kutupiana shutuma jumatatu juu ya kuendelea kwa ghasia katika eneo lenye utajiri wa mafuta la  Abyei ambalo linapiganiwa kati ya mpaka wa kaskazini na kusini.
Msemaji wa umoja wa mataifa Martin Nesirky amesema askari walinda amani wa umoja wa mataifa wameongeza doria katika eneo la Abyei. Amesema umoja wa mataifa umeguswa sana na ghasia na wapo katika hatua ya kuthibitisha idadi ya majeruhi.

0 comments:

WELCOME URARY95 SPORTS NEWS BLOG | ADVERTISE YOUR BUSINESS HERE AT A CHEAP PRICE MORE INFORMATION CONTACT US: 0654315901 | Email: urary95@yahoo.com | KARIBU URARY95 SPORTS NEWS BLOG | TANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA GHARAMA NAFUU KWA MAELEZO ZAIDI WASILIANA NASI: 0654315901 | Barua Pepe: urary95@yahoo.com
 
Back to top!