Searching...
Thursday, January 27, 2011

Ahadi pekee hazitoshi kuimarisha afya ya wanawake na watoto asema mkuu wa UM

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon amerejea msimamo wake wa kuimarisha afya ya wanawake na watoto .
Ban Ki-moon Geneva
Ban Ki-moon Geneva
Ban amesema mkakati uliozinduliwa karibuni wa kuimarisha afya ya wanawake na watoto umepata msaada wa fedha wa dola milioni 40. Ameongeza kuwa ingawa fedha ni nyenzo muhimu kwa mkakati huo lazima kuwe na uwajibikaji na uwazi kwa matumizi ya fedha hizo. Katibu Mkuu ameyasema hayo hii leo mjini Geneva wakati wa mkutano wa kwanza wa tume ya uwajibikaji kwa ajili ya afya na wanawake na watoto.

Tume ya uwajibikaji kwa ajili ya afya ya wanawake na watoto ilianzishwa mwaka 2010 kufuatilia msaada kwa ajili ya wanawake na watoto jinsi unavyotumika na endapo matokeo yanayotarajiwa yanapatikana. Mwekiti wa tume hiyo ni Rais wa Tanzania Jakaya Kikwete na waziri mkuu wa Canada Stephen Harper.

0 comments:

WELCOME URARY95 SPORTS NEWS BLOG | ADVERTISE YOUR BUSINESS HERE AT A CHEAP PRICE MORE INFORMATION CONTACT US: 0654315901 | Email: urary95@yahoo.com | KARIBU URARY95 SPORTS NEWS BLOG | TANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA GHARAMA NAFUU KWA MAELEZO ZAIDI WASILIANA NASI: 0654315901 | Barua Pepe: urary95@yahoo.com
 
Back to top!