Baadhi ya wasanii wanaopendwa sana nchini Nigeria - D'banj, Onyeka Onwenu, Zaaki Azzay, Twoshotz - wote wanaimba kumuunga mkono Rais Goodluck Jonathan.
Lakini si wote wanaocheza.
Msanii wa miondoko ya Afrobeat Seun Kuti anaghadhibishwa.
"Yeyote anayetumia musiki wake kuunga mkono wanasiasa wa Nigeria ni msaliti - kwanza anausaliti muziki na pili anaisaliti nchi yake."
Maisha
Wakati mabilioni ya dola za mafuta yanapotelea katika akaunti za benki za wanasiasa wakubwa nchini Nigeria kila mwezi, zaidi ya asilimia 70 ya wananchi wanapambana na maisha kwa chini ya dola moja kwa siku.Uchaguzi ujao wa urais umepangwa kufanyika Aprili 9 2011, na harakati za kampeni zimeshika kasi.
"Muziki ni moja ya silaha kuu ambayo inatakiwa kulikomboa bara hili," anasema Kuti.
"ninapoona sasa muziki unatumika kukandamiza, unatumika dhidi ya watu, kwa kweli ni makosa."
Utamaduni mzito wa Nigeria wa harakati kwa kutumia muziki umetiwa doa.
Mashairi yake yenye kuona mbele yalikebehi uroho wa wanasiasa, kulaani ghasia zinazofanywa na polisi, na kupinga udhibiti uliokuwepo, ili kusema yanayotendeka.
Niliahidiwa fedha nyingi ambazo sijawahi kuona, na mmoja wa wagombea urais
Banky W
"Niliahidiwa fedha nyingi ambazo sijawahi kuona, na mmoja wa wagombea urais," anasema Banky, huku akionekana kushangazwa.
Lakini aligoma kuzichukua.
"Ni muhimu kwetu sisi wenye sauti ya umma, kujaribu kuipeleka nchi mahala tunapodhani inatakiwa kwenda, vinginevyo tutakabiliana na matatizo yale yale, miaka 20 ijayo, kwa sababu hakuna aliyesimama kuitetea nchi."
Kupokea fedha
Wasanii wengi ambao wametoa nyimbo za kampeni, wamekataa kuzungumzia wazi wazi kuhusu mikataba walioingia na wanasiasa."Tulikuwa na imani kuwa wimbo wetu utapeleka ujumbe, kuwahamasisha watu kwenda kupiga kura," amesema.
Mashabiki wengi
Mwanamuziki mwingine Zaaki Azzay, ambaye amerekodi wimbo maalum wa Bw Jonathan, amekana kupokea fedha zozote kwa kumuunga mkono."Si kwa sababu za fedha. Naunga mkono sera za Bw Jonathan, na mabadiliko ambayo naamini anaweza kuyaleta," anasema.
"Wataalam wengi wanafikiri vijana hawajitokezi kupiga kura, lakini wasanii hawa wana mashabiki wengi," anasema Abidemi Dairo, mwandishi wa muziki mjini Lagos.
"Iwapo Goodluck Jonathan atajaribu kuwa nao karibu, ana nafasi kubwa ya kupata ushindi," anaamini mwandishi huyo.
Mara ya mwisho kwa wasanii kuwa pamoja kwa mtindo huu, kuunga mkono wanasiasa, ilikuwa zaidi ya miaka kumi iliyopita.
Licha ya kujitetea kuwa walifanya maonesho kwa kulazimishwa, wengi wa waliopigwa picha wakishiriki katika hafla hiyo, walipatwa na matatizo katika fani yao, na hawakurejea tena katika umaarufu.
Katika nchi ambayo wastani wa umri ni miaka 19, Wanigeria wengi - hasa ambao wanacheza muziki katika kumbi za usiku - ni wadogo mno kukumbuka yaliyotokea kipindi hicho.
Ni wazi kuwa wanasiasa wanaelewa vilivyo kuwepo kwa idadi kubwa ya Wanigeria vijana, na wana hamu ya kutumia mgongo wa mafanikio waliyoyapata waimbaji na wasanii wa hip-hop.
Lakini iwapo wimbo mzuri utabadili mawazo ya mpiga kura, hilo ni suala jingine.
Afrika Mashariki
Wimbi la matumizi ya muziki katika siasa limefika pia Afrika Mashariki.Katika uchaguzi ambao ulionekana ukiwa wa kupambana vikali kwa mara ya kwanza katika siasa za vyama vingi, bila shaka kila mbinu ilitumika.
Kama ilivyo Nigeria, muziki wa kisasa ambao una wafuasi wengi vijana nchini Tanzania ulitumika vilivyo kuwavuta wapiga kura wakati wa kampeni.
Mikataba
Baadhi ya waimbaji walibadili mashairi ya nyimbo zao ambazo zinapendwa na kupachika mashairi ya kusifia vyama vya kisiasa, wagombea na sera.Tofauti kidogo na Nigeria, baadhi ya wasanii wa Tanzania waligombea nafasi za uongozi katika vyama vya kisiasa.
Hata hivyo suala la uwazi wa mikataba na malipo kwa wasanii pia halikuwa likizungumzwa wazi wazi.
Msanii wa muziki maarufu wa Bongo Flavour, Inspekta Haroun, akizungumza na BBC wakati wa kampeni za uchaguzi Tanzania, alisema anashiriki katika kupigia debe chama kinachotawala - Chama Cha Mapinduzi (CCM) - kwa sababu anapenda sera zake na ana imani na wagombea wake.
"Mimi silipwi chochote ninapoburudisha mashabiki katika mikutano ya kampeni, nafanya hivyo kwa mapenzi ya chama changu" alisema Inspekta.
Katika moja ya tamasha la chama chake cha NRM wasanii kadhaa maarufu kama vile Eddy Kenzo na GNL Zamba walipamba jukwaa.
Hata hivyo, katika kuzitaka kura za vijana, Rais Museveni mwenyewe amediriki kuimba.
"Hatuna budi kuezi utamaduni wetu" alisema Bw Museveni na kuongeza "tutunze mashairi yetu katika nyimbo zetu ili yasisahaulike. Tunayahitaji mashairi hayo".
Mashairi
Mashairi anayozungumzia na aliyoyatumia ni ya nyimbo za kitamaduni alizokuwa akiimba wakati akiwa mdogo.Mashairi hayo baadaye yalichukuliwa na watayarishaji wa muziki, yakachanganywa na midundo ya kisasa na wimbo kamili kutolewa unaojulikana kama 'You want another rap?.
Wimbo huo umekuwa maarufu nchini Uganda, ukipigwa katika kumbi za starehe na hata kutumiwa kama mlio wa simu.
Katika uchaguzi wa Rwanda na Burundi ambao umefanyika mwaka 2010, muziki hata hivyo haukuwa na nafasi kubwa.
Je Kenya inayotarajia kufanya uchaguzi wake mwaka 2012, itafuata mkondo huohuo wa siasa kutumia muziki?
Ni jambo la kusubiri.
0 comments:
Post a Comment