Searching...
Tuesday, December 7, 2010

Shirikisho la Wachina wanaoishi magharibi mwa Afrika laanzishwa

Balozi Deng Boqing
Shirikisho la Wachina wanaoishi katika sehemu ya magharibi mwa Afrika limeanzishwa tarehe 5 huko Lagos, Nigeria.
Balozi wa China nchini Nigeria na kwenye Jumuiya ya uchumi ya nchi za Afrika Magharibi ECOWAS Deng Boqing amesema katika muda mrefu uliopita, Wachina wanaoishi magharibi mwa Afrika wametoa mchango mkubwa katika kuhimiza urafiki na kuimarisha ushirikiano wa kiuchumi kati ya China na Afrika. Vitega uchumi vinavyowekezwa na Wachina hao vimetoa nafasi za ajira elfu 40 huko, thamani ya biashara kati ya China na Afrika inatarajiwa kuzidi dola za kimarekanili bilioni 7.5.

0 comments:

WELCOME URARY95 SPORTS NEWS BLOG | ADVERTISE YOUR BUSINESS HERE AT A CHEAP PRICE MORE INFORMATION CONTACT US: 0654315901 | Email: urary95@yahoo.com | KARIBU URARY95 SPORTS NEWS BLOG | TANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA GHARAMA NAFUU KWA MAELEZO ZAIDI WASILIANA NASI: 0654315901 | Barua Pepe: urary95@yahoo.com
 
Back to top!