Searching...
Wednesday, December 22, 2010

Baridi kali iliyoikumba Ulaya kupungua kidogo: WMO

Utabiri wa hali ya hewa unaonyesha kwamba hali ya baridi kupindulia inayoathiri sehemu za Ulaya Magharibi na Mashariki mwa Marekani itapungua katika siku chache zijazo.
Nembo ya WMO
Nembo ya WMO
Kwa mujibu wa shirika la kimataifa la utabiri wa hali ya hewa WMO ingawa baridi kali sio kitu kigeni kwa majira kama haya ni vigumu kutabiri hali hii ya hewa ya kupindukia itaendelea kwa muda gani. Maelfu ya wasafiri wamekwama katika viwanja mbalimbali vya ndege barani Ulaya ambao barabu inayomwagika kwa wingi imeathiri usafiri katika kipindi ambacho kila mwaka kinakuwa na kinapilika nyingi. Claire Nullis ni afisa katika shirika la WMO.
WMO inasema hali mbaya ya hewa kama hii ilishuhudiwa pia mwaka 2009, hata hivyo limesema si kawaida kushuhudia tukio hilo katika miaka miwili mfululizo.

0 comments:

WELCOME URARY95 SPORTS NEWS BLOG | ADVERTISE YOUR BUSINESS HERE AT A CHEAP PRICE MORE INFORMATION CONTACT US: 0654315901 | Email: urary95@yahoo.com | KARIBU URARY95 SPORTS NEWS BLOG | TANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA GHARAMA NAFUU KWA MAELEZO ZAIDI WASILIANA NASI: 0654315901 | Barua Pepe: urary95@yahoo.com
 
Back to top!