Searching...
Wednesday, November 24, 2010

Maambukizi mapya ya virusi vya HIV na ukimwi yanapungua duniani:UNAIDS

Idadi ya watu wapya wanaoambukizwa virusi vya HIV na ukimwi inapungua kwa mujibu wa ripoti iliyotolewa na mpango wa pamoja kupambana na ukimwi wa Umoja wa Mataifa UNAIDS.
Ripoti ya kimataifa ya ukimwi
Ripoti ya kimataifa ya ukimwi
Watu takribani milioni 2.6 waliambukizwa virusi vya HIV mwaka 2009 idadi ambayo ni ndogo kwa asilimia 20 ikilinganishwa na miaka kumi iliyopita. UNAIDS inasema hali hiyo inaambatana pia na kupungua kwa vifo vitokanavyo na maradhi yanayohusiana na ukimwi ambayo kwa mwaka jana wa 2009 vilikuwa milioni 1.8 ikilinganishwa na vifo milioni 2.1 mwaka 2004.
Mkurugenzi mkuu wa UNAIDS Michel Sidibe anasema uwekezaji katika kukinga na mipango ya tiba unazaa matunda, lakini juhudi zaidi zinahitajika.

UNAIDS inasema ufadhili wa kimataifa wa mipango ya tiba na kinga kwa virusi vya HIV na ukimwi unapungua na usipoangaliwa kwa makini basi unaweza kugeuza mafanikio yaliyoaanza kupatikana.

0 comments:

WELCOME URARY95 SPORTS NEWS BLOG | ADVERTISE YOUR BUSINESS HERE AT A CHEAP PRICE MORE INFORMATION CONTACT US: 0654315901 | Email: urary95@yahoo.com | KARIBU URARY95 SPORTS NEWS BLOG | TANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA GHARAMA NAFUU KWA MAELEZO ZAIDI WASILIANA NASI: 0654315901 | Barua Pepe: urary95@yahoo.com
 
Back to top!