Searching...
Monday, October 11, 2010

Kenya yawafukuza waalimu kwa kuharibu watoto

Mwanafunzi wa shule moja Kenya akifanya uchoraji.
Mwanafunzi wa shule moja Kenya akifanya uchoraji.
Maafisa wa Kenya wanasema zaidi ya waalimu 1,000 wamefukuzwa kazi katika kipindi cha miaka miwili iliyopita kwa sababu ya kufanya mapenzi na wasichana wanafunzi.

Maafisa wa elimu wanasema waalimu hao wamefukuzwa kwa kuwapa mimba wanafunzi wa shule na vitendo vingine vya ngono. Matukio mengi yamefanyika katika shule za msingi za umma.

Pamoja na kufukuzwa kazi, baadhi ya waalimu wanakabiliwa na mashitaka ya jinai katika mahakama.
Maafisa wanasema zaidi ya waalimu 500 wamefukuzwa kazi mwaka huu kwa kuhusika na unyanyasaji wa ngono na kwamba waalimu 600 waliachishwa kazi mwaka jana.

0 comments:

WELCOME URARY95 SPORTS NEWS BLOG | ADVERTISE YOUR BUSINESS HERE AT A CHEAP PRICE MORE INFORMATION CONTACT US: 0654315901 | Email: urary95@yahoo.com | KARIBU URARY95 SPORTS NEWS BLOG | TANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA GHARAMA NAFUU KWA MAELEZO ZAIDI WASILIANA NASI: 0654315901 | Barua Pepe: urary95@yahoo.com
 
Back to top!