Searching...
Friday, September 24, 2010

Obama: Afrika iwe muuzaji chakula nje

Rais Barack Obama
Rais Barack Obama akihutubia kikao cha 65 cha Umoja wa Mataifa Septemba 23, 2010.
"Hakuna sababu Afrika isiwe muuzaji mkubwa wa chakula nje," Obama
Rais Barack Obama wa Marekani amezitaka nchi za Afrika kufanya juhudi na kuwa wauzaji wakubwa wa chakula nje ya nchi kote duniani.
Akihutubia mkutano mkuu wa Umoja wa Mataifa mjini New York Alhamisi rais Obama alisema "hakuna sababu Afrika isiwe muuzaji mkubwa wa chakula nje." Aliongezea kuwa ndio sababu ameweka mipango nchini mwake ambaye itawezesha wakulima barani Afrika.
Alisema Marekani inafanya juhudi kuifanya dunia iwe wazi zaidi, na kuwezesha biashara na kuinua uchumi wa nchi zote duniani kwa ushirikiano katika nyanja zote. Alisema hakuna sababu kwa mfanyabiashara kulipa rushwa akitaka kufungua biashara, na kukumbusha kuwa wajibu wa serikali ni kuwezesha wananchi sio kuwabana.

0 comments:

WELCOME URARY95 SPORTS NEWS BLOG | ADVERTISE YOUR BUSINESS HERE AT A CHEAP PRICE MORE INFORMATION CONTACT US: 0654315901 | Email: urary95@yahoo.com | KARIBU URARY95 SPORTS NEWS BLOG | TANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA GHARAMA NAFUU KWA MAELEZO ZAIDI WASILIANA NASI: 0654315901 | Barua Pepe: urary95@yahoo.com
 
Back to top!