Searching...
Thursday, July 1, 2010

Utamaduni ni kuhusu kuhodhi mabadiliko asema mkuu wa UNFPA

Mkuu wa shirika la Umoja wa Mataifa la idadi ya watu UNFPA Thoraya Ahmet Obaid amesema utamaduni ni kuhusu kuhodhi mabadiliko na hakuna mabadiliko yatakayokuja kutoka nje.

Utamaduni

Utamaduni

Obaid alikuwa akizungumza katika mjadala wa kwanza kabisa wa moja kwa moja wa televisheni na kuongeza kuwa tamaduni zina nguvu kuliko utekelezaji wa sheria.
Ameelezea thamani ya jinsi utamaduni unavyompa hadhi mwanamke akihoji kwamba kama wanawake hawana haki za msingi kama kuzaa na afya ya uzazi watawezake kuwa na sauti kuhusu hatma yao?

Washiriki wengine katika mjadala huo ni pamoja na mkurugenzi wa UNESCO Irina Bokova na walijadili uhusiano baina ya utamaduni na hadhi ya mwanamke, na kuangalia jinsi masuala ya uchumi, siasa na kijamii yanavyoathiri kuwawezesha wanawake.

0 comments:

WELCOME URARY95 SPORTS NEWS BLOG | ADVERTISE YOUR BUSINESS HERE AT A CHEAP PRICE MORE INFORMATION CONTACT US: 0654315901 | Email: urary95@yahoo.com | KARIBU URARY95 SPORTS NEWS BLOG | TANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA GHARAMA NAFUU KWA MAELEZO ZAIDI WASILIANA NASI: 0654315901 | Barua Pepe: urary95@yahoo.com
 
Back to top!