Searching...
Tuesday, July 20, 2010

Ingawa hatua zimepigwa lakini bado vita dhidi ya ukimwi vinakabiliwa na changamoto:Ban

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon amesema kumepigwa hatua kubwa kimataifa kukabiliana na HIV na ukimwi.

Mkutano wa ukimwi

Mkutano wa ukimwi

Ban ameyasema hayo katika ujumbe maalumu kwa njia ya video kwenye mkutano wa kimataifa wa ukimwi ulioanza jana mjini Vienna Austria. Ban amesema maambukizi mapya yamepungua, wigo wa kuweza kupata dawa umeongezeka na vikwazo vya usafiri kwa waathirika vinaondolewa. Lakini ameonya kuwa pamoja na mafanikio bado kuna vikwazo vingi, kwani kuna baadhi ya serikali zinapunguza bajeti za kupambana na ukimwi.

Amesema hatua hiyo inatia hofu na amewataka wote kuhakikisha kwamba mafanikio yaliyopatikana katika vita hivyo hayageuki. Naye Michel Sidibe mkurugenzi wa shirika la Umoja wa Mataifa la kupambana na ukimwi UNAIDS akizungumza kwenye mkutano huo amesema ana imani kuwa kwa pamoja dunia inaweza kutokomeza ugonjwa wa ukimwi

0 comments:

WELCOME URARY95 SPORTS NEWS BLOG | ADVERTISE YOUR BUSINESS HERE AT A CHEAP PRICE MORE INFORMATION CONTACT US: 0654315901 | Email: urary95@yahoo.com | KARIBU URARY95 SPORTS NEWS BLOG | TANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA GHARAMA NAFUU KWA MAELEZO ZAIDI WASILIANA NASI: 0654315901 | Barua Pepe: urary95@yahoo.com
 
Back to top!