Searching...
Monday, July 5, 2010

NONDOZZZZ HYDERABAD!!!

Ni siku ya furaha katika maisha ya wahitimu waliomaliza shahada zao za kwanza kwa elimu ya juu hapa Hyderabad,India.Wakirusha kofia zao juu kuashiria kuhitimu kwao
Wahitimu wakipata picha ya pamoja na Mgeni Rasmi Pr.V.RAMA RAO mkuu wa chuo cha Aptech India nzima pamoja na Mwenyekiti wa Jumuiya ya Watanzania wote waishio Hyderabad Bw.ABDILLAH D. NKYA.
Picha za pamoja ulikuwa ni mtindo wa kubadilishana nafasi kama unavyoonekana hili wote wapate nafasi ya kupata kumbukumbu

Bw.NASSIB IBRAHIM ama Nass kama anayojulikana akionesha cheti chake alichotunikiwa kwa kuwa mwandaaji wa jarida maalumu kwa wahitimu kwa mwaka huu
Kwanza toka kushoto ni Bw.MUSTAFA SAID a.k.a Matata akiwa na Bw.NASSIB pamoja na Bw.SADDALLAH R. MBEYU wakipata kumbukumbu ya pamoja katika maafali hayo
Mimi nikiwa na Bw.Matata nikipata kumbukumbu nae
Bw.Matata akipokea cheti chake kwa ishara ya amani na upendo
Bw.Nass nae akipokea chati chake kwa kuwa mwanafunzi wa kwanza kwa kuandaa jarida kwa wahitimu kitu ambacho hakijawahi kutokea katika historia ya wanafunzi wasomao hapa hyderabad,kazi nzuri sana
Bw.Khalid Said Bahasan ni mmoja ya wahitimu kwa mwaka huu akipokea cheti chake toka kwa mgeni rasmi
Bw.Saddallah Mbeyu akionesha cheti chake juu kwa ishara ya hiki hapa cheti jamani oneniiii
Bw.Saddallah Mbeyu akiwa na Bw.Matata katika picha ya pamoja wakiwa ndani ya ukumbi wa maafali huku wakisikiliza nini kinaendeleaa toka kwa mshereheshaji
Mwenyekiti wa Jumuiya ya wanafunzi wanaoishi hapa Hyderabad Bw.ABDILLAH D. NKYA akiwa na Mgeni Rasmi katika maafali Pr.V RAMA RAO

Baadhi ya sehemu ya wageni waalikwa waliofika katika maafali hayo pia wakiwa ni wanafunzi waliohudhuria kwa kuwasindikiza wahitimu kwa kumaliza mda wao wa masomo hapa Hyderabad,India.
Ulikuwa ni mda wa kuimba wimbo wa Taifa wa Tanzania kama ilivyokawaida katika kila shughuli zetu tulisimama kwa kuimba kwa pamoja
Baadhi ya sehemu ya wageni waalikwa wakiimba wimbo wa Taifa wa Tanzania
Wahitimu nao wakiimba wimbo wa Taifa kwa pamoja
Wahitimua wakiwa katika nyuso za tabashashi kabisaa katika kuimba wimbo wa Taifa
Baadhi ya wahitimu wakiimba wimbo wa Taifa kwa heshima zote
Mwenyekiti wa Jumuiya wa Watanzania akiwa na Mgeni Rasmi mbele kabisa wakiwa katika heshima zote kwa kuimba wiimbo wa Taifa
Bw.Saddallah Mbeyu
Wahitimu wakiwa kimya nia baada ya kumaliza kuimba wimbo wa Taifa
Mbele kabisa Bi.FATMA SALUM akifuatiwa na Bi.KHADIJA NASSOR wakiwa katika nyuso za furaha kabisa katika kuwasindikiza wahitimu
Bw.Nass akitafakari jambo na Bw.Deuce Majige katika maafali hayo
Bw.Shakir wa kwanza toka kushoto akiwa na Bw.Ibrahimu wakipata kumbukumbu ya pamoja katika maafali hayo hapa ni nje ya ukumbi
Hawa ni baadhi ya wahitimu mbele kabisa ni Bw.Walid akifuatiwa na Bw.Anwar mwisho wao ni Bw.Daniel Masimbusi

Bw.Nass akiwa katika pozi ni nje ya ukumbi
Mimi nikipata kumbukumbu ya pamoja na mmoja wa wahitimu Bw.Anwar na mwisho kabisa ni Bw.Nass
Mbele kabisa ni Bw.Abdu aziz akifuatiwa na Bw.Walid na mwisho kwa mbali ni Bw.Noor wakipata chai ndani ya ukumbi
Hawa nia wadau wangu wakuu
Bw.Nass akiwa na Bw.Khalid ni kabla ya maafali.
Mwisho kabisa nawatakieni kila la kher wahitimu wote kwa kumaliza salama muda wenu wote wa masomo na kufanikiwa kuhitimu nawatakieni maisha mema huko muendako na huu uwe ndio mwanzo wa safari yenu msihishie hapa,M/MUNGU awabariki wote!!!!

0 comments:

WELCOME URARY95 SPORTS NEWS BLOG | ADVERTISE YOUR BUSINESS HERE AT A CHEAP PRICE MORE INFORMATION CONTACT US: 0654315901 | Email: urary95@yahoo.com | KARIBU URARY95 SPORTS NEWS BLOG | TANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA GHARAMA NAFUU KWA MAELEZO ZAIDI WASILIANA NASI: 0654315901 | Barua Pepe: urary95@yahoo.com
 
Back to top!