Searching...
Monday, June 21, 2010

UNCTAD imewataka washirika wa biashara Afrika kulisaidia bara hilo katika usafirishaji nje wa bidhaa zake

Ripoti mpya kuhusu mfumo wa biashara Afrika inaonya kuwa kukuwa kwa maingiliano ya biashara na nchi kubwa zilizoendelea zikiwemo China, India, na Brazil, hakujalisaidia bara hilo kusafirisha bidhaa zinazoliongezea faida.

Ripoti hiyo mpya ya mkutano wa Umoja wa Mataifa kuhusu biashara na maendeleo UNCTAD inasema ongezeko la ushirikiano wa kibiashara eneo la Kusini kunaweza kulisaidia bara la Afrika sio tuu kwa kukuza biashara na kiwango cha fedha lakini pia kusaidia miundombinu ya eneo hilo na kuwapa ujuzi na teknolojia.

Katibu Mkuu wa UNCTAD Supachai Panitchpakdi, amesema hata hivyo mfumo wa biashara na uwekezajipande wa kusini unaimarisha mfumo wa muda mrefu ambapo nchi za Afrika zinasafirisha nje bidhaa za kilimo, madini, chuma, na mafuta yasiyosafishwa na zinaingiza bidhaa zilizokwisha tengenezwa

0 comments:

WELCOME URARY95 SPORTS NEWS BLOG | ADVERTISE YOUR BUSINESS HERE AT A CHEAP PRICE MORE INFORMATION CONTACT US: 0654315901 | Email: urary95@yahoo.com | KARIBU URARY95 SPORTS NEWS BLOG | TANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA GHARAMA NAFUU KWA MAELEZO ZAIDI WASILIANA NASI: 0654315901 | Barua Pepe: urary95@yahoo.com
 
Back to top!