Searching...
Thursday, June 24, 2010

Kuna ongezeko la matumizi ya mihadarati katika nchi zinazoendelea: UNODC

Ripoti ya kimataifa ya dawa za kulevya kwa mwaka huu 2010 inaonyesha matumizi ya dawa hizo yanahamia kwenye dawa mpya na masoko mapya.

Matumizi ya mihadarati

Matumizi ya mihadarati

Ripoti hiyo iliyotolewa leo na ofisi ya umoja wa Mataifa ya madawa na uhalifu UNODC inasema usambazaji wa kimataifa wa aina mbili za dawa zenye matatizo opiates na cocaine unaendelea kupungua.
Pia imebaini katika miaka miwili iliyopita ardhi iliyokuwa ikitumika kwa kilimo cha mimea ya kutengeneza dawa hizo duniani kote imepungua kwa asilimia 23. Lakini imeonya kuwa watumiaji wa dawa mpya aina ya amphetamine ni kati ya milioni 30 na 40 na idadi hiyo inazidi ile ya watuamiaji wa opiate na cocaine kwa pamoja.
Mkuu wa UNDOC Antonio Maria Costa amesema hatuwezi kutatua tatizo la dawa za kulevya kama tunabadili aina ya dawa kutoka heroine na cocaine na kuanza kutumia dawa zingine za kulevya ambazo pia zina madhara.

0 comments:

WELCOME URARY95 SPORTS NEWS BLOG | ADVERTISE YOUR BUSINESS HERE AT A CHEAP PRICE MORE INFORMATION CONTACT US: 0654315901 | Email: urary95@yahoo.com | KARIBU URARY95 SPORTS NEWS BLOG | TANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA GHARAMA NAFUU KWA MAELEZO ZAIDI WASILIANA NASI: 0654315901 | Barua Pepe: urary95@yahoo.com
 
Back to top!