Searching...
Friday, June 4, 2010

Bw. Ban Ki-Moon ashtushwa na tukio la kuuawa kwa Bw. Floribert Chebeya

Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Bw. Ban Ki-Moon tarehe 3 Juni alitoa taarifa akieleza kushtushwa na tukio la kuuawa kwa Bw. Floribert Chebeya ambaye ni mwanaharakati maarufu wa haki za binadamu nchini Jamuhuri ya kidemokrasia ya Congo, pia alisisitiza kuwa ni lazima kufanya uchunguzi ulio wazi na huru juu ya tukio hilo.

Kwenye taarifa hiyo Bw. Ban Ki-Moon alisema, Bw. Floribert Chebeya akiwa kiongozi wa harakati za kutetea haki za binadamu wa Jamhuri ya kidemokrasi ya Congo anaheshimiwa na jumuiya ya kimataifa na ndugu zake, na kazi alizozifanya zikiwa ni alama ya moyo thabiti wa watu wa nchi hiyo zitakumbukwa na watu.

Bw. Ban Ki-Moon pia alisema, Umoja wa Mataifa unajiandaa kutoa msaada kwa ajili ya uchunguzi wa tukio hilo kupitia Tume maalumu ya Umoja wa Mataifa nchini Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo

0 comments:

WELCOME URARY95 SPORTS NEWS BLOG | ADVERTISE YOUR BUSINESS HERE AT A CHEAP PRICE MORE INFORMATION CONTACT US: 0654315901 | Email: urary95@yahoo.com | KARIBU URARY95 SPORTS NEWS BLOG | TANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA GHARAMA NAFUU KWA MAELEZO ZAIDI WASILIANA NASI: 0654315901 | Barua Pepe: urary95@yahoo.com
 
Back to top!