Searching...
Monday, May 31, 2010

Mahakama ya ICC kujadiliwa Uganda.

Ocampo akiwa na Waziri Mkuu wa Kenya Raila Odinga

Ocampo akiwa na Waziri Mkuu wa Kenya Raila Odinga


Wajumbe kutoka zaidi ya nchi 100 wanakutana mjini Kampala Uganda, kujadili mafanikio ya Mahakama ya Kimataifa ya jinai ICC, tangu ilipobuniwa miaka minane iliyopita.

Mahakama hiyo kwa sasa inaendesha uchunguzi wa kesi tano kuu, zote kuhusu washukiwa kutoka barani Afrika.

Hadi kufikia sasa mahakama hiyo haijatoa hukumu yoyote dhidi ya mshukiwa yeyote, ingawa mwendesha mkuu wa mashtaka, Luis Moreno-Ocampo, amefahamisha BBC kuwa kuwepo kwa mahakama hiyo kumebadili ambavyo majeshi, serikali na hata mahakama za nchi tofauti zinavyoendesha harakati zao.

Kongamano hilo pia litajadili uwezekano wa kufanyia mabadiliko sheria za makubaliano ya Rome yaliyopelekea kundwa kwa mahakama hiyo miaka kumi na mbili iliyopita.

Habari na Bbcswahili

0 comments:

WELCOME URARY95 SPORTS NEWS BLOG | ADVERTISE YOUR BUSINESS HERE AT A CHEAP PRICE MORE INFORMATION CONTACT US: 0654315901 | Email: urary95@yahoo.com | KARIBU URARY95 SPORTS NEWS BLOG | TANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA GHARAMA NAFUU KWA MAELEZO ZAIDI WASILIANA NASI: 0654315901 | Barua Pepe: urary95@yahoo.com
 
Back to top!