KLABU
ya Manchester United imemtambulisha rasmi mshambuliaji Radamel Falcao
baada ya kukamilisha uhamisho wake katika siku ya mwisho ya kufungwa
pazia la usajili.
Mpachika
mabao huyo wa Monaco aria wa Colombia aliwasili kwa ndege binafsi
kusaini mkataba wa mkopo wa muda mrefu wa msimu Old Trafford kwa ada ya
Pauni Milioni 6, ambao unatoa fursa ya kununuliwa moja kwa moja kwa
Pauni Milioni 46.
Falcao ameiambia www.manutd.com:
"Nina furaha kujiunga na Manchester United kwa mkopo msimu huu.
Manchester United ni klabu kubwa duniani na wazi inatakiwa kurudi
juu,"amesema mchezaji huyo ambaye ameweka wazi hamu yake ya kufanya kazi
na kocha Louis van Gaal ili kutoa mchango wake kuirudisha juu klabu hiyo.
Falcao akiwa ameshika kwa pamoja jezi ya United na kocha Msaidizi wa timu hiyo, Ryan Giggs
Nyota huyo wa Colombia anakuwa mchezaji wa nane kutoka nchi hiyo kucheza Ligi Kuu ya England
0 comments:
Post a Comment