Searching...
Thursday, July 31, 2014

MAREFA LIGI KUU ENGLAND MSIMU UJAO MAMBO SAFI KAMA KOMBE LA DUNIA BRAZIL

New: The Premier League have confirmed that referees will use vanishing spray this season
Mpya: Viongozi wa ligi kuu nchini England wamethibitisha kutumia dawa ya kutoweka iliyotumika katika fainali za kombe la dunia nchini Brazil.

DAWA ya kutoweka iliyotumika kuweka alama ya kuta za ulinzi kwenye michuano ya kombe la dunia itatumika katika michuano ya ligi kuu soka nchini England msimu ujao.
Dawa hiyo ya kupulizia inayotoweka haraka itatumiwa na waamuzi ili kuwaweka wachezaji umbali wa mita 10 kutoka kwenye mpira wakati wa upigaji wa mipira iliyokufa.
Clever: The 'magic spray' is used to mark free-kicks and prevent player encroachment
Hapa mchezaji hana ujanja wa kudanganya
 

Mkurugenzi mkuu wa bodi ya ligi kuu nchini England, Richard Scudamore alisema: 'Siku zote tunafuata maendeleo yanayoongeza ushindani na ni wazi tulitazama kombe la dunia na kuona dawa ya kutoweka ikiwasaidia waamuzi, wachezaji na wengine wote wanaotazama mechi,'

"Dawa hiyo itatumika pia kwenye mechi za ligi ya mabingwa na ligi ya Europa, lakini kwa mechi za ligi itajaribiwa kwa  kwenye mechi ya kombe la  Johnstone’.
Chama cha soka, FA, kinatarajia kupelekea ombi kwenye kamati ya kombe la FA ili kutumia dawa hiyo.
Dawa hii itatumika kwenye mechi ya kufungua msimu wa ligi kuu baina ya Manchester United na Swansea, agosti 16 mwaka huu.
Elite: The spray will also be used by UEFA in the Champions League and Europa League
Mwisho hapa, sawa?

0 comments:

WELCOME URARY95 SPORTS NEWS BLOG | ADVERTISE YOUR BUSINESS HERE AT A CHEAP PRICE MORE INFORMATION CONTACT US: 0654315901 | Email: urary95@yahoo.com | KARIBU URARY95 SPORTS NEWS BLOG | TANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA GHARAMA NAFUU KWA MAELEZO ZAIDI WASILIANA NASI: 0654315901 | Barua Pepe: urary95@yahoo.com
 
Back to top!