MKONGWE Didier Drogba ametimiza ndoto zake za kurejea Chelsea.
Nyota
huyo wa Ivory Coast amesaini Mkataba wa mwaka mmoja Stamford Bridge, na
kuwa gwiji wa klabu hiyo baada ya awali kusajiliwa na Jose Mourinho kwa
Pauni Milioni 24 mwaka 2004. Na Drogba amesema asingeweza kukataa fursa ya kufanya kazi na Mreno huyo tena.
"Ulikuwa
ni uamuzi rahisi - Nisingekataa fursa ya kufanya kazi na Jose tena.
Kila mmoja anafahamu uhusiano maalum nilionao na klabu hii na wakati
wote nahisi kama nyumbani kwangu.
Kushoto anapima afya na kulia anasaini mkataba wa mwaka mmoja
Kwa
upande wake, Mourinho amesema hana wasiwasi Drogba ataisaidia Chelsea,
kwa sababu bado anaamini ni mmoja wa washambuliaji duniani.
"Anakuja
kwa sababu ni mmoja wa washambuliaji bora Ulaya. Nafahamu
haiba yake vizuri sana na nafahamu kama akirudi hatalindwa na historia
au kile alichokifanya katika klabu hii mwanzo," amesema Mourinho.
0 comments:
Post a Comment