Manchester United imefungua majadiliano na klabu ya Sporting Lisbon juu ya uhamisho wa kiungo mkabaji wa William Carvalho.
Meneja
wa United David Moyes anaaminika kumuweka kiungo huyo mwenye miaka 21
katika listi ya wachezaji atakaowasajili kipindi dirisha la usajili
litakpofunguliwa, hii ni kwa mujibu wa taarifa za usajili barani ulaya.
Klabu
ya Ureno imepanga kiasi cha €35million (£29m) kwa timu yoyote
itakayomtaka kiungo huyo ambaye ana asili ya Angola, lakini United wapo
tayari kulipa kiasi cha €35million.
Lakini kwa kuwa United wanataka kumaliza biashara yao ya usajili mapema kabla ya kuanza kwa michuano ya kombe la dunia, wanaweza wakakubali kulipa fedha wanayotaka.
0 comments:
Post a Comment