Hizi
ni fainali za 20 za kombe la dunia, zijue timu zilizowahi kutwaa
ubingwa wa kombe la dunia pamoja na wafungaji wa michuano hiyo kuanzia
mwaka 1930 mpaka 2010.
Mwaka
1930 fainali ziliandaliwa nchini Uruguay wakati mfungaji bora wa
michuano hiyo alikuwa Muargentina Guillermo Stabile aliefunga magoli
nane wakati bingwa wa kombe la dunia mwaka huo ilikuwa ni timu ya taifa
ya Uruguay,.
Fainali
za pili za dunia zilifanyika mwaka 1934 nchini Italy huku Old rich
Nejedly akitwaa kiatu cha dhahabu na Italy walitawaa taji la ubingwa wa
dunia.
Fainali
za tatu zilifanyika mwaka 1938 nchini Ufaransa wakati Leonidas wa
Brazil alitwaa kiatu cha ufungaji bora Italy walitetea taji la kombe la
dunia.
Fainali
za nne zilifanyika nchini Brazil mwaka 1950 , mfungaji bora alikuwa
mbrazil Admir aliefunga magoli 8, wakati mabingwa walikuwa ni nchi ya
Uruguay.
Fainali
za tano zilifanyika mwaka 1954 nchini Switzerland mfungaji bora
alikuwa Sandor Kocsis wa Hungary aliefunga magoli 11, kwa mara ya kwanza
Ujerumani Magharibi walitwaa kombe la dunia.
Fainali
za sita zilifanyika mwaka 1958 nchini Sweden, mfungaji bora alikuwa
mchezaji wa kimataifa wa Ufaransa Just Fontaine aliefunga magoli 13,
wakati Brazil walikuwa mabingwa kwa mara ya kwanza.
Fainali
za saba zilifanyika mwaka 1962 nchini Chile, wafungaji bora walikuwa
Drazan Jerkovic wa Czesk, Florian Albert wa Hungary, Garrincha wa
Brazil, leonel Sanchez wa Chile, Valentin Ivanov wa Russia, na Vava wa
Brazil wote walifunga magoli manne kila mmoja, wakatI Brazil
walifanikiwa kutwaa taji la dunia kwa mara ya pili.
Fainali
za nane zilifayika mwaka 1966 nchini England, mfungaji bora alikuwa ni
mreno Eusebio ambaye alifunga magoli 9, huku England kwa mara ya kwanza
wakatwaa taji hilo la dunia.
Fainali
za tisa zilifanyika nchini Mexico mwaka 1970, mfungaji bora alikuwa ni
Gerd Muller alifunga magoli 10, na timu ya taifa ya Brazil ama Selcao
walitwaa taji la dunia.
Fainali
za kumi zilifanyika mwaka 1974 nchini Ujerumani Magharibi, mfungaji
bora Grzegorz Lato wa Poland aliefunga magoli saba, kwa mara ya pili
Ujerumani Magharibi walitwaa kombe la dunia.
Fainali
za kumi na moja zilifanyika nchini Argentina mwaka 1978, Mario Kempes
wa Argentina alikuwa mfungaji bora baada ya kufunga magoli sita, pia
Argentina walitwaa taji hilo la dunia kwa mara ya kwanza.
Fainali
za kumi na mbili zilifanyika mwaka 1982 nchini Hispania , mfungaji bora
alikuwa Paulo Rossi aliefunga magoli sita na na timu ya taifa ya Italy
maarufu kama Azuri walitwaa ubingwa wa dunia kwa mara ya pili.
Fainali
za kumi na tatu zilifanyika mwaka 1986, nchini Mexico, mfungaji bora
alikuwa Gary Lineker wa England baada ya kufunga magoli sita, na
Argentina walitwaa ubingwa wa dunia kwa mara ya pili.
Fainali
za kumi na nne zilifanyika nchini Italy, mwaka 1990, mfungaji bora
alikuwa Salvatore Schillaci wa Italy aliefunga magoli sita, na timu ya
Ujerumani Magharibi wakatwaa ubingwa.
Fainali
za kumi na tano zilifanyika nchini Marekani mwaka 1994, wafungaji bora
walikuwa Hrist Stoichkov, Oleg Salenko wa Russia baada ya kufunga magoli
sita, kila mmoja, na Brazil walifanikiwa kutwaa ubingwa wa dunia.
Fainali
za kumi na sita zilifanyika nchini Ufaransa mwaka 1998, mfungaji bora
alikuwa Davor Suker alitwaa kiatu cha ufungaji bora, na timu ya taifa ya
Ufaransa ilitwaa ubingwa wa Dunia.
Fainali
za kumi na saba ziliandaliwa na nchi mbili za bara la Asia, kwenye nchi
za Korea Kusini na Japan mfungaji bora alikuwa ni Ronaldo de Lima wa
Brazil aliefunga magoli nane, wakati Brazil walifanikiwa kutwaa taji la
dunia kwa mara ya tano.
Fainali
za kumi na nane ziliandaliwa nchini Ujerumani mwaka 2006, mfungaji bora
wa michuano hiyo alikuwa Miroslav Klose baada ya kufunga magoli matano,
huku Italy wakitwaa ubingwa wa dunia kwa mara ya nne.
Fainali
za kumi na tisa ziliandaliwa nchini Afrika Kusini mwaka 2010, wafungaji
bora walikuwa Diego Forhan wa Uruguay, Thomas Muller wa Ujerumani,
Wesley Sneider wa Uholanzi, na David Villa wa Hispania, bingwa wa
alikuwa timu ya taifa ya Hispania maarufu kama La Roja.
0 comments:
Post a Comment