Searching...
Wednesday, April 24, 2013

MAUAJI YA KUTISHA CHUO CHA UHASIBU -ARUSHA


Huyu Ndio Henry Aliye Uawa


Mbunge Wa Arusha Mjini Godbless Lema Akiwatuliza Wanafunzi Wa Chuo Hicho



Taarifa Kutoka  Chuo Cha Uhasibu Arusha zinadai kuwa Mwanafunzi Wa BEF 2  anayejulikana  kwa  jina  la  Henry  ameuawa  kikatili  na  watu  wasiofahamika....

Mwanafunzi  huyo  Alikuwa Masomoni Mida Ya Usiku Na Alipomaliza Aliondoka Na Kuelekea Maeneo Ya Esami. Kabla Hajafika Eneo La Malazi (Hostel) alipigiwa Simu na Mwenzake amsubiri Ili Waende Wote Hostel.    
 Inasemekana Wakati anamsubiri Rafiki Yake Kwenda Hostel, Kuna Bajaj Ilifika Eneo Hilo Na Watu Hao Wasiojulikana Wakataka Pesa Kutoka Kwa Mwanafunzi Huyo...Wakati  wakiendelea  kuzozana, rafiki  yake  naye  alifika.....  
Majibu Ya Wanafunzi Hao Hayakuwafurahisha Watu Hao Na Ndio Walipochomoa Kisu Na Kumchoma Mmoja wa Vijana Hao Tumboni Na Shingoni na Kupoteza Maisha Hapo Hapo....  
Rafiki Aliye Kuwa Nae Inasemekana Alichomwa Kisu Cha Tumboni Na Kuachwa Akishuhudia Mwenzake Akipoteza Maisha.
Edited:by Abuu

0 comments:

WELCOME URARY95 SPORTS NEWS BLOG | ADVERTISE YOUR BUSINESS HERE AT A CHEAP PRICE MORE INFORMATION CONTACT US: 0654315901 | Email: urary95@yahoo.com | KARIBU URARY95 SPORTS NEWS BLOG | TANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA GHARAMA NAFUU KWA MAELEZO ZAIDI WASILIANA NASI: 0654315901 | Barua Pepe: urary95@yahoo.com
 
Back to top!