MKUU wa Mkoa wa Arusha, Magesa Mulongo
ameamuru polisi kumkamata Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema pamoja
na wanafunzi walioshiriki kurusha mawe baada ya kutokea vurugu
zilizotokana na kifo cha mwanafunzi wa mwaka wa pili, Chuo cha Uhasibu
Arusha, Henry Kago (22).
Naibu Mkuu wa Chuo cha Uhasibu Arusha,
Faraji Kasidi jana alitangaza kufunga chuo hicho kwa muda usiojulikana
kutokana na vurugu zilizotokea chuoni hapo, ikiwemo ukiukwaji wa nidhamu
na urushwaji wa mawe uliofanywa na wanafunzi hao kwa Mkuu wa Mkoa na
kamati ya ulinzi na usalama.
Mulongo alitoa amri hiyo baada ya Lema kudaiwa kuingia chuoni hapo jana asubuhi na kufanya siasa bila kufuata utaratibu.
“Si jambo jema kwa Mbunge kuingia chuoni
na kuhamasisha siasa kwenye jambo hilo la kifo badala ya kuwatuliza
wanafunzi ili tujue kiini cha tatizo hili," alisema mkuu wa mkoa na
kushutumu kwamba jambo hilo linabadilika badala ya msiba linawekwa chuki
za siasa na wanafunzi nao kuingia kwenye mkumbo.
Kwa mujibu wa mkuu wa mkoa, upo utata wa
kifo cha Kago kutokana na wengine kudai ameuliwa na bodaboda eneo la
Esami na Kanisa la Waadventista Wasabato karibu na chuo huku wengine
wakidai alitoka eneo la Bugaluu.
Alisema polisi inachunguza utata wa kifo hicho cha mwanafunzi huyo aliyekutwa na simu yake ya mkononi.
"Naagiza polisi kumkamata Lema popote
alipo na wanafunzi wengine pamoja na wakili wake,” alisema Mkuu wa Mkoa
bila kutaja jina la wakili.
Kwa mujibu pia wa RADIO FIVE ya jijini
Arusha, Mkuu huyo wa mkoa wa Arusha bwana Mulongo amenukuliwa kwa nyakati tofauti tangu jana akitaja
uwezekano wa
Lema kusababisha kifo cha mwanafunzi ili apate nafasi ya kufanya siasa
chuoni hapo.
Edited:by ABUU
0 comments:
Post a Comment