Searching...
Wednesday, April 24, 2013

CHELSEA NDIO TIMU YA MWISHO KUIFUNGA BARCA MABAO 4 KWENYE CHAMPIONS LEAGUE: MESSI ANA NUKSI NA MULLER

* Mara ya mwisho mshambuliaji Lionel Messi kuichezea timu iliyofungwa mabao 4-0 ilikuwa dhidi ya wajerumani. Argentina ilipofungwa kwenye robo fainali ya kombe la dunia 2010. Pia siku hiyo kama ilivyokuwa leo Thomas Mueller, alifunga mabao mawili tena.

* Barcelona wameruhusu wavu wao kuguswa mara nne katika mechi ya Champions League kwa mara ya kwanza tangu walipofungwa 4-2 na Chelsea katika hatua ya 16 bora March 2005.


* Timu ya kwanza kuifunga Barcelona 4-0 katika michuano ya ulaya ilikuwa ni Dynamo Kiev katika hatua ya makundi mnamo November 1997.


* Hakuna timu iliyofungwa kwenye raundi ya kwanza ya hatua ya mtoano ya Champions League/European Cup kwa mabao manne kwa bila au zaidi iliyoweza kufuzu kuendelea raundi ya pili.


* Barcelona walipiga shuti moja tu liloenga goli la Bayern leo, idadi ndogo zaidi katika Champions League msimu huu.


* Katika mashindano yote - Barcelona hawajafungwa 4-0 tangu walipoonyoshwa na Getafe katika kombe la mfalme May 2007. Miaka sita iliyopita.

 
Edited:by Abuu

0 comments:

WELCOME URARY95 SPORTS NEWS BLOG | ADVERTISE YOUR BUSINESS HERE AT A CHEAP PRICE MORE INFORMATION CONTACT US: 0654315901 | Email: urary95@yahoo.com | KARIBU URARY95 SPORTS NEWS BLOG | TANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA GHARAMA NAFUU KWA MAELEZO ZAIDI WASILIANA NASI: 0654315901 | Barua Pepe: urary95@yahoo.com
 
Back to top!