Searching...
Tuesday, September 25, 2012

Serengeti Fiesta 2012 Iringa hiyooooooo inawashika usiku huu

Uzao wa THT, na huyu ni mwadada machachari anaekuja kwa kasi Rachel, akipagawisha juu ya jukwaa madhubuti la  SERENGETI FIESTA 2012 ndani ya uwanja wa Samora mjini Iringa hivi sasa. 
 Bongo movie wakiwa jukwaani
 Shilole akiserebuka
 Aunt Ezekiel we acha tu
 Ray huyoooo akikamua
 Wema nae aliimba za Diamond
 Diamond akikamua jukwaani
Sheta akimchezesha Diamond
 
Msanii funga kazi wa Hip Hop, Roma Mkatoliki akikamua jukwaani kwa staili yake ya kidole cha mwisho juu, Tamasha la Serengeti Fiesta 2012, ndani ya uwanja wa Samora mjini Iringa usiku huu.
 Msanii wa Kizazi kipya Ben Paul akifanya makamuzi yake ndani ya Uwanja wa Samora mjini Iringa katika tamasha la Serengeti Fiesta 2012
 Linah akiimba mbele ya mashabiki wake usiku huu ndani ya tamasha la Serengeti Fiesta 2012 mjini Iringa
 Nimakamuzi ya kiutu uzima kutoka kwa Linah ambaye pia ni zao la THT.
 Mkali Stamina nae akifanya makamuzi jukwaanikatika show kali ya Serengeti Fiesta Iringa usiku huu wa Septemba 23/24 uwanja wa Samora
 DJ PQ akifanya makamuzi yake stegini
 Mwanadada Linah akifanyiwa mahojiano na mtangazaji wa Clouds TV, Nickson ambaye anawika katika Kipindi chake cha Weekend Chart Show!
Hapa wakazi wa Iringa wakimwangalia Tausi, mwana dada ambaye naweza kusema ni mfupi kuliko wote ambao nimekwisha wahi kuwaona maishani mwangu.
Mkali Lenex akifanya vitu vyake jukwaani, hakika Serengeti Fiesta Iringa ni Bhaaaaass!!
Haya sasa MC wa Show Baba Johnniiiie!! akifanya kazi yake na kukubalika na mashabiki hapo chini.

Ni mkali mwingine kutoka jijini Mwanza kupitia shindano la Serengeti Supa Nyota 2012, Young  KIller akikamua vilivyo mbele ya wakazi wa mji wa Iringa wanaondelea kutinga hivi sasa ndani ya uwanja wa samora,kutibwirika pamoja na muonekano mpya wa tamasha la Serengeti Fiesta 2012.
Ni mkali mwingine kutoka Morogoro kupitia shindano la Serengeti Supa Nyota 2012,Jo Maker akikamua vilivyo mbele ya wakazi wa mji wa Iringa wanaonelea kuingia hivi sasa ndani ya uwanja wa samora,kutibwirika pamoja na muonekano mpya wa tamasha la Serengeti Fiesta 2012.
Mmoja wa wasanii chipukizi aliyeibukia kwenye shindano la Serengeti Supa Nyota 2012,kutoka Mkoani Mbeya aitwaye Ney Lee pichani akionesha kipaji chake cha kuimba jukwaani usiku huu kwenye uwanja wa Samora,mkoani Iringa ambako hivi sasa kunarindima tamasha la Serengeti Fiesta 2012.

 
Wadau wa Serengeti fiesta Iringa na Dar es Salaam nao wapo hapa Uwanja wa Samora Iringa kupata burudani
Ndani ya uwanja wa Samora Mjini Iringa ndo kwaaaanza kumekucha katika tamasha kubwa na la aina yake ya SERENGETI FIESTA 2012 ambapo linajiachia usiku huu hadi Bhaaaaaass!!
Wameanza kupanda wasanii chipukizi wa mjini Iringa na vitongoji vyake.
 Watu ndo nao kama hivi nab ado wanamiminika uwanjani.
Kama hujafika uwanjani hapa fika sasa

0 comments:

WELCOME URARY95 SPORTS NEWS BLOG | ADVERTISE YOUR BUSINESS HERE AT A CHEAP PRICE MORE INFORMATION CONTACT US: 0654315901 | Email: urary95@yahoo.com | KARIBU URARY95 SPORTS NEWS BLOG | TANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA GHARAMA NAFUU KWA MAELEZO ZAIDI WASILIANA NASI: 0654315901 | Barua Pepe: urary95@yahoo.com
 
Back to top!