Searching...
Wednesday, June 6, 2012

Uingereza yakamilisha kilele cha sherehe za utawala wa Malkia

              
Maelfu ya wakazi wa jiji la London walihudhuria sherehe kubwa kwenye uwanja wa Kasri ya Buckingham, makazi rasmi ya Malkia, kwa siku ya mwisho ya sherehe za miaka 60 za utawala wa Malkia Elizabeth wa pili wa Uingereza.

Malkia Elizabeth mwenye umri wa miaka 86 na familia yake waliwapungia mikono wakazi wa London huku wakipeperusha bendera za nchi hiyo kutoka kwenye eneo la nje Jumanne wakati ndege ya kifalme ikiruka angani.


Wakati huo huo Rais Barack Obama wa Marekani alitoa salamu binafsi kwa malkia akisema anamatumaini ataendelea kuongoza na kuwa na afya salama kwa miaka mingi ijayo. Katika video iliyotolewa kwenye tovuti ya White House bwana Obama alimuita malkia “living witness” kwa kuboresha uhusiano maalumu kati ya Uingereza na Marekani, dhamana ambayo alisema inabaki kuwa muhimu sana kwa nchi zao hizo mbili na dunia.

0 comments:

WELCOME URARY95 SPORTS NEWS BLOG | ADVERTISE YOUR BUSINESS HERE AT A CHEAP PRICE MORE INFORMATION CONTACT US: 0654315901 | Email: urary95@yahoo.com | KARIBU URARY95 SPORTS NEWS BLOG | TANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA GHARAMA NAFUU KWA MAELEZO ZAIDI WASILIANA NASI: 0654315901 | Barua Pepe: urary95@yahoo.com
 
Back to top!