Searching...
Thursday, June 14, 2012

OFFICIAL: DI MATTEO APEWA MIAKA MIWILI KUIONGOZA CHELSEA


Roberto Di Matteo leo amethibitishwa kuwa kocha mpya wa kudumu wa Chelsea kwa mkataba wa miaka miwili.

Muitaliano huyo alirudi Stamford Bridge leo akitokea kwenye mapumziko na kukamilisha dili  hilo na mabingwa wa ulaya.

Di Matteo alisema: "Nina furaha kuweza kuchaguliwa kuwa manager mpya. Tulipata mafanikio makubwa msimu uliopita ambayo yalijenga historia kwenye klabu.
"Lengo letu ni kuendelea kutokea hapo tulipofika na tayari nimeanza kupanga maandalizi ya msimu ujao."

Di Matteo, 42, alitajwa kama kocha wa muda wa Chelsea baada ya Andre Villas Boas kufukuzwa kazi mwezi wa 3.

Akafanikiwa kuiongoza The Blues kushinda  kombe la FA na champions league ndani ya kipindi cha wiki 11.

0 comments:

WELCOME URARY95 SPORTS NEWS BLOG | ADVERTISE YOUR BUSINESS HERE AT A CHEAP PRICE MORE INFORMATION CONTACT US: 0654315901 | Email: urary95@yahoo.com | KARIBU URARY95 SPORTS NEWS BLOG | TANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA GHARAMA NAFUU KWA MAELEZO ZAIDI WASILIANA NASI: 0654315901 | Barua Pepe: urary95@yahoo.com
 
Back to top!