Katika
kuendeleza ushirikiano na uhusiano wa uchumi na biashara kati ya China
na nchi za Afrika, na kuonyesha bidhaa za Kichina katika soko la Afrika,
serikali ya China imeandaa maonyesho ya ‘Brands of China African
Showcase 2012’ ambayo ni maonyesho ya kwanza ya aina hii kufanyika
Afrika nzima.
Hafla
hii imeandaliwa na Wizara ya Biashara ya Jamhuri ya Watu wa China,
Serikali za majimbo ya Jiangsu, Zhejiang na Guangdong ambayo itafanyika
kuanzia tarehe 1 hadi 5 Julai 2012 katika maonyesho ya kimataifa ya Dar
es Salaam maarufu kama sabasaba.
Maonyesho
haya yatachukua ukubwa wa mita 2,600 za mraba, vibanda 150 na
exhibitors 110 kutoka mikoa 8 ya China. Maonyesho haya yamegawanya
katika makundi manne kulingana na bidhaa ambazo ni; mashine, magari,
vifaa vya umeme, vifaa vya nyumbani, vyombo vya mawasiliano,
elektroniki, nishati ya jua, bidhaa za matumizi ya kila siku, vifaa vya
ujenzi, , kemikali , huduma za afya na bidhaa za kisasa.
Sherehe
ya Ufunguzi wa Brands of China African Showcase 2012 itafanyika tarehe 2
Julai 2012, kuanzia saa 9.00 mchana katika viwanja vya maonyesho vya
sabasaba na imeandaliwa na Wizara ya Biashara ya Jamhuri ya Watu wa
China.
Kadika
siku tano za maonyesho, Kongamano kati ya kampuni hizi za kiChina na
wafanyabiashara wa Afrika utafanyika ili kutoa nafasi ya exhibitors na
wanunuzi kuzungumza uso kwa uso, na kubadilishana mawazo na mbinu za
kibiashara.
Katika miaka ya hivi karibuni, China imezidi kuboresha uwezo wa kiuchumi, kisayansi na ugunduzi.
Mauzo
ya nje ya China kwa Afrika imekuwa imara katika ubora, bei na huduma.
China imefanya mchango chanya katika kutengeneza bidhaa zinazotimiza
mahitaji ya watu wa Afrika, ili kuboresha hali ya maisha ya umma kwa
ujumla na jitihada za kuinua uchumi wa ndani na maendeleo ya kijamii
Waonyeshaji
bidhaa hao 110 kutoka China watakaofanya maonyesho wamechaguliwa kwa
makini sana na mwandaaji wa maonyesho. Makampuni haya yamechaguliwa
kutokana na kuwa na uzoefu wa miaka mingi katika mauzo ya nje na pia
yanaaminika na kusaidia jamii. Makampuni haya yanajulikana kwa kutoa
bidhaa zenye ubora imara zinazotambuliwa na kupokelewa duniani kote.
Maonyesho
haya yanatoa nafasi kubwa kwa bidhaa za Kichina kuonyeshwa Afrika, na
hivyo kuwezesha watu wa Afrika kufahamu vizuri bidhaa za Kichina. Hii
ni nafasi muhimu kwa wanabiashara wa Afrika kufanya ushirikiano wa
kibiashara na makampuni yanayotambulika China ili kupata faida kwa pande
zote mbili.
0 comments:
Post a Comment