Searching...
Thursday, May 17, 2012

WANAMICHEZO,WANAMUZIKI WAMLILIA MAFISANGO


Wachezaji Haruna Niyonzima wa Yanga kushoto na Uhuru Selemani wa Simba wakisikitika wasijue la kufanya baada ya kushuhudia mwili wa mchezaji mwenzao marehemu Patrick Mafisango katika chumba cha kuhifadhia maiti muhimbili leo.
Mbunge wa jimbo la Korogwe CCM Steven Ngonyani Prof Maji Marefu akizungumza na wanahabari hospitalini hapo kuelezea masikitiko yake juu ya kifo cha mchezaji huyo.
Haruna Moshi akitoka kwenye chumba cha kuhifadhia maiti huku akilia kwa uchungu baada ya kuhakikisha kweli mwenzao Patrick Mafisango amefariki.
Hapa Haruna Moshi akihojiwa alijaribu kuongea lakini akashindwa.
Mchezaji Uhuru Selemani akilia kwa uchungu huku akifarijiwa na mmoja wa waombolezaji.
Mchezaji wa zamani wa Simba Boniface Pawasa akilia kwa uchungu huku akifarijiwa na Mchezaji haruna Niyonzima wa Yanga, Pawasa amesema jana walikuwa naye kwenye muziki katika klabu ya Maisha Oysterbay wakati bendi ya Akudo Impact ikifanya onyesho klabuni hapo na marehemu alimuaga kwamba anaenda nyumbani baadae akapigiwa simu kwa simu ya marehemu akiambiwa mwenye simu hii amefariki dunia kwa ajali.
Boniface Pawasa kushoto, Uhuru Selemani wakilia.
Uhuru Selemani akisalimiana na wanamuziki wa bendi ya Akudo Impact ambao pia wameelezaea masikitiko yao kwani wamesema marehemu walikuwa naye usiku wa kuamkia leo katika klabu ya Maisha ambako walikuwa wakifanya onyesho lao.
Aliyewahi kuwa mchezaji wa timu ya Simba Mrundi Ramadhana Wasso akihojiwa na waandishi wa habari kuelezea masikitiko yake kutokana na msiba huo.
Mashabiki wa Simba wakiwa katika hospitali ya Muhimbili kwa masikitiko makubwa kwa kuondokewa na mchezaji wao kipenzi.
Baadhi ya waandishi wa habari wakiwa katika chumba cha kuhifadhia maiti kwenye hospitali ya taifa ya Muhimbili leo asubuhi.

0 comments:

WELCOME URARY95 SPORTS NEWS BLOG | ADVERTISE YOUR BUSINESS HERE AT A CHEAP PRICE MORE INFORMATION CONTACT US: 0654315901 | Email: urary95@yahoo.com | KARIBU URARY95 SPORTS NEWS BLOG | TANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA GHARAMA NAFUU KWA MAELEZO ZAIDI WASILIANA NASI: 0654315901 | Barua Pepe: urary95@yahoo.com
 
Back to top!