Searching...
Sunday, June 19, 2011

Spurs haitamuuza Modric

Mwenyekiti wa klabu ya soka ya Tottenham Hotspur inayocheza katika ligi kuu ya Premier ya England, Daniel Levy, amesema klabu hakina nia ya kumuuza Luka Modric kwa "bei yoyote ile".
Kiungo cha kati Modric, kutoka Croatia, ameonyesha nia ya kutaka kujiunga na wapinzani Chelsea, pia katika ligi kuu ya Premier.
Luka Modric
Anataka kujiunga na Chelsea pasipo kuwaudhi Spurs
Chelsea wako tayari kutoa kitita cha pauni milioni 22.
Modric, mwenye umri wa miaka 25, bado hajawasilisha ombi rasmi la kutaka kuondoka uwanja wa White Hart Lane, lakini inaelekea angelipenda kuendelea kucheza soka mjini London.
"Ningelipenda kwenda Chelsea," alielezea, "lakini ningelipenda kuwaacha Spurs kama marafiki".

0 comments:

WELCOME URARY95 SPORTS NEWS BLOG | ADVERTISE YOUR BUSINESS HERE AT A CHEAP PRICE MORE INFORMATION CONTACT US: 0654315901 | Email: urary95@yahoo.com | KARIBU URARY95 SPORTS NEWS BLOG | TANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA GHARAMA NAFUU KWA MAELEZO ZAIDI WASILIANA NASI: 0654315901 | Barua Pepe: urary95@yahoo.com
 
Back to top!