Rais wa shirikisho la soka nchini Afrika Kusini, (Safa) amesema taifa hilo liko tayari kuchukua mahala pa Libya na kuwa mwenyeji wa fainali za kombe la taifa bingwa barani afrika mwaka wa 2013.
Nematandani amesema Safa litaiandikia CAF baadaye wiki hii kuwasilisha nia yake.
Mapema mwaka huu, Afrika Kusini, iliandaa fainali za kuwania fainali zakombe la taifa bingwa barani Afrika kwa wavulana wasiozidi umri wa miaka 20 baada ya maandamano ya kisiasa kuanza nchini Libya.
Baadaa ya kuandaa fainali za kombe la dunia mwaka uliopita, AfrikaKusini, tayari imepangiwa kuwa mwenyeji wa fainali hizo mwaka wa 2017.
Uamuzi huo sasa huenda ukanyeuka ikiwa CAF itaamua kuwa fainali za mwaka wa 2013 zitaandiliwa nchini humo, lakini Nematandani amesema wao wako tayari kwa mashauriano zaidi.
Afrika Kusini iliwania nafasi ya kuandaa fainali hizo za mwaka wa 2015 lakini CAF ikaamua nafasi hiyo kutwaliwa na Morocco.
0 comments:
Post a Comment