Taarifa iliyotolewa baada ya mazungumzo hayo inasema, kamati hiyo itaundwa na wanasheria na wanasiasa kabla ya mwezi Machi. Taarifa imesema, makundi ya upinzani yamekubali rais Mubarak kutogombea tena urais mwezi Septemba, na kuhakikisha mpito wa amani na uchaguzi mkuu utafanyika kwa uhuru na haki.
Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon amesema mchakato wa kukabidhiana madaraka nchini Misri unapaswa kuamuliwa na wananchi wa nchi hiyo na ufanyike kwa amani na utaratibu, ili kuepusha kuvuruga amani na utulivu katika Mashariki ya Kati.


0 comments:
Post a Comment