Searching...
Wednesday, December 1, 2010

UM umezindua ombi kuwasaidia watu milioni 50 duniani

Umoja wa Mataifa unaomba dola bilioni 7.4 ili kukidhi gharama za operesheni zake za kibinadamu kwa mwaka 2011.
Waathirika wa njaa
Waathirika wa njaa
Fedha hizo zinatarajiwa kushughulikia matatizo makubwa 14 ya kibinadamu duniani kote ambako watu zaidi milioni 50 wameathirika. Mratibu wa masuala ya kibinadamu wa Umoja wa Mataifa Valarie Amos anasema vita na majanga ya asili bado yanatawala maisha ya watu wengi katika nchi zilizoathirika, yakiwalazimisha kuzihama nyumba zao huku wakikosa huduma muhimu kama maji ya kunya na huduma za afya.

Nchi 28 zitanufaika na ombi hilo la msaada wa 2011.Sudan ndio itakayopata sehemu kubwa ya fedha hizo dola bilioni 1.7, ikifuatiwa na Haiti ambayo itapokea dola milioni 907 na kisha Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo ambayo itapata dola milioni 719.

0 comments:

WELCOME URARY95 SPORTS NEWS BLOG | ADVERTISE YOUR BUSINESS HERE AT A CHEAP PRICE MORE INFORMATION CONTACT US: 0654315901 | Email: urary95@yahoo.com | KARIBU URARY95 SPORTS NEWS BLOG | TANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA GHARAMA NAFUU KWA MAELEZO ZAIDI WASILIANA NASI: 0654315901 | Barua Pepe: urary95@yahoo.com
 
Back to top!