Alhamisi, Rais Barack Obama alifanya mazungumzo yaliyohusu maswala mengi na Rais wa China Hu Jintao na Chansella wa Ujerumani Angela Merkel. Katika taarifa fupi baada ya mkutano wao Rais Obama alisema Rais Hu hakusema lolote kuhusu mgogoro wao juu ya sera za sarafu ya China, swala kubwa katika uhusiano wa China na Marekani.
Rais Obama alisema Marekani na China zinaona maendeleo makubwa katika maswala mbali mbali kati yao, na zina wajibu mahsusi kuhakikisha ukuaji wa uchumi katika nchi zao. Rais Hu alisema China iko tayari kushirikiana na Marekani kuongeza mazungumzo na ushirikiano baina yao.
0 comments:
Post a Comment