Searching...
Wednesday, October 6, 2010

UN yasisitiza kiongozi wa waasi anayekabiliwa na tuhuma za kunajisi watu Congo ametiwa nguvuni

Ofisi ya Umoja wa Mataifa katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo imesisitiza kuwa kiongozi wa kundi la waasi wa Mai Mai Luteni Kanali Mayele anayekabiliwa na tuhuma zakushambulia raia na kubakwa wanawake 500 ametiwa nguvuni. Luteni Kanali Mayele alitiwa nguvuni mapema jana huko mashariki mwa Congo.
Mjumbe wa Umoja wa Mataifa nchini Congo amekaribisha kutiwa nguvuni kwa kiongozi wa kundi la Mai Mai Cheka akisema kuwa ni ushindi wa haki na uadilifu. Margot Wallstrom ambaye ni mtaalamu wa masuala ya ubakaji anayetembelea Congo amesema kutiwa nguvuni Kanali Mayele ni ushindi mkubwa wa uadilifu hususan kwa wanawake waliobakwa na kunajisiwa. Amesema kuwa kutiwa nguvuni mhalifu huyo ni ishara kwamba wahalifu wengine hawataweza kukimbia mkono wa uadilifu.
Kiongozi wa kundi la Mai Mai Cheka Luteni Kanali Mayele anatuhumia kwamba aliongoza kundi la watu mia mbili na wapiganaji wa Kihutu kutoka Rwanda katika mashambulizi yaliyolenga vijiji 13 vya eneo la Walikale katika jimbo la Kivu Kusini ambapo wanawake 500, watoto wadogo na hata wanaume walibakwa na kunajisiwa. Hujuma hiyo ilifanyika katika kipindi cha mwishoni mwa mwezi Julai hadi mwanzoni mwa Agosti.

0 comments:

WELCOME URARY95 SPORTS NEWS BLOG | ADVERTISE YOUR BUSINESS HERE AT A CHEAP PRICE MORE INFORMATION CONTACT US: 0654315901 | Email: urary95@yahoo.com | KARIBU URARY95 SPORTS NEWS BLOG | TANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA GHARAMA NAFUU KWA MAELEZO ZAIDI WASILIANA NASI: 0654315901 | Barua Pepe: urary95@yahoo.com
 
Back to top!