Searching...
Tuesday, October 5, 2010

Ujumbe wa baraza la usalama kuzuru nchini Uganda na Sudan

Baraza la usalama la Umoja wa Mataifa leo limekutana kujadili masuala yatakayomulikwa katika mwezi huu wa Oktoba ambapo Uganda ndiye Rais wa baraza hilo.
Dr. Ruhakana Rugunda wa Uganda
Dr. Ruhakana Rugunda wa Uganda
Balozi wa Uganda kwenye Umoja wa Mataifa Ruhaganda Rugunda akizungumza na idhaa hii amesema kwa mwezi mzima vikao vya baraza la usalama vitaghubikwa na masuala ya afrika.

Rugunda ambaye ataongoza vikao vyote vya baraza la usalama kwa mwezi huu amesema suala la kura ya maoni ya Sudan litasalia kwa muda kwenye baraza hilo ikiwa na mambo ningine ya Afrika kwa sababu ni bara linalozongwa na matatizo mengi

0 comments:

WELCOME URARY95 SPORTS NEWS BLOG | ADVERTISE YOUR BUSINESS HERE AT A CHEAP PRICE MORE INFORMATION CONTACT US: 0654315901 | Email: urary95@yahoo.com | KARIBU URARY95 SPORTS NEWS BLOG | TANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA GHARAMA NAFUU KWA MAELEZO ZAIDI WASILIANA NASI: 0654315901 | Barua Pepe: urary95@yahoo.com
 
Back to top!