Searching...
Tuesday, October 19, 2010

Kiongozi wa Upinzani Rwanda Mahakamani

Ingabire amefikishwa mahakamani kwa tuhuma za uhaini
Kiongozi wa Chama cha upinzani nchini Rwanda, FDU Inkingi, Ingabire Victoire amefikishwa mbele ya mahakama na kusomewa mashtaka mapya ya uhaini.
Ingabire alikamatwa wiki iliyopita kwa tuhuma za uhaini na kushirikiana na makundi ya kigaidi kuhujumu usalama wa Rwanda.
Upande wa mashtaka umeelezea kwamba Bi Ingabire alikamatwa baada ya madai yaliyotolewa na mwanajeshi wa zamani Meja Vital Uwumuremyi, aliyekamatwa mnamo Jumatano wiki iliyopita.
Mwanajeshi huyo wa zamani anadaiwa kuwapa maafisa wa upelelezi fununu kwamba alipata msaada kutoka kwa mwanasiasa huyo kubuni kikundi cha kijeshi cha chama hicho cha FDU.
Madai haya yamekanushwa na vyama vya upinzani nchini humo.
Mwanasiasa huyo alirejea nchini Rwanda kutoka ushamishoni kwa lengo la kugombea kiti cha urais katika uchaguzi uliofanyika Agosti mwaka huu.
Watetezi wa haki za binadamu wanailaumu serikali ya Rwanda kwa kuwakandamiza wapinzani.
Hata hivyo Rais Paul Kagame amekuwa akikanusha madai haya kwa kusema kuwa serikali yake inatawala kwa misingi ya haki na haitaruhusu mtu yeyote kuvuruga amani.

0 comments:

WELCOME URARY95 SPORTS NEWS BLOG | ADVERTISE YOUR BUSINESS HERE AT A CHEAP PRICE MORE INFORMATION CONTACT US: 0654315901 | Email: urary95@yahoo.com | KARIBU URARY95 SPORTS NEWS BLOG | TANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA GHARAMA NAFUU KWA MAELEZO ZAIDI WASILIANA NASI: 0654315901 | Barua Pepe: urary95@yahoo.com
 
Back to top!