Searching...
Friday, September 24, 2010

Mahakama ya Kenya yawapata na hatia ya uharamia Wasomali 7

 Sample ImageMahakama ya Mombasa nchini Kenya imewapata na hatia ya kufanya uharamia Wasomalia 7 na kuwahukumu kifungo cha miaka mitano jela kwa kuteka nyara meli ya Uhispania mwaka 2009. Wasomalia hao wamehukumiwa baada ya kutiwa mbaroni mwezi Mei mwaka uliopita. Suala la kuwahukumu maharamia wa Kisomali wanaokamatwa limekuwa likikwamishwa na kuzusha hitilifau za mitazamo juu ya nchi gani wahukumiwe maharamaia hao. Somalia yenyewe haina vyombo vya sheria vya kuendesha kesi hizo. Kenya ina wasiwasi kuwa maharamia wanaoachiliwa baada ya kutumikia vifungo vyao jela na wale wasiopatikana na hatia watalundikana nchini humo, na suala hilo kuhatarisha usalama wa nchi hiyo. Kuna maharamia wa Kisomali 15 wanaotumikia kifungo nchini Kenya huku mamia ya wengine bado wakiwa wanaendelea kushikiliwa.

0 comments:

WELCOME URARY95 SPORTS NEWS BLOG | ADVERTISE YOUR BUSINESS HERE AT A CHEAP PRICE MORE INFORMATION CONTACT US: 0654315901 | Email: urary95@yahoo.com | KARIBU URARY95 SPORTS NEWS BLOG | TANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA GHARAMA NAFUU KWA MAELEZO ZAIDI WASILIANA NASI: 0654315901 | Barua Pepe: urary95@yahoo.com
 
Back to top!