Searching...
Wednesday, August 4, 2010

UCHAGUZI 2010/ PIGA KURA



Princess Lumy
Kumi na minane ili kuweza kupiga kura
Ni haki ya juu hata weusi waamerika
Leo ni zamu yako dada, kaka kuchagua
Kura yako ndio sauti yako

Mchokozy Ahmedinho

Milolongo vituoni, wameacha zao kazi.
Kura zao mikononi, kuchagua viongozi.
Watujenge maishani, vifaidike vizazi.
mwanati huonekani, kumbe we wakuna nazi?

Princess Lumy

Kamwe huwezi daiwa, mwananchi yako haki
Jiandikishe ka dawa, chukua nafasi kiki
Faida ni yako daima, usitafute bunduki
Ndugu wa Tanzania, mda huo wa mikiki

Mafisadi tumewachoka, nchi yetu kuangamia
Viwango bora kuvifika, kama we wazingatia
Piga kura dada kaka, usije kuugulia
Kilichobaki ni kura yako maana ndio sauti yako

Mchokozy Ahmedinho

Chagua alo na sera, si asali mdomoni.
Mwanadada fanya ghera, utumbukize debeni.
Usihongwe kwa madera, yaso faida mbeleni.
Haki yako piga kura, uwakilishwe bungeni.


Sa usipopiga wewe, mwewe ndo atachukua
Usipatwe na kiwewe, anza mapema chagua
Hii yako dira uwe, maisha bora kupanga
Mi naongea na wewe, piga kura dada kaka

1 comments:

princesslumy said...

Wonderful!!!!!
Yes, YES WE CAN
Time to vote Tanzania

WELCOME URARY95 SPORTS NEWS BLOG | ADVERTISE YOUR BUSINESS HERE AT A CHEAP PRICE MORE INFORMATION CONTACT US: 0654315901 | Email: urary95@yahoo.com | KARIBU URARY95 SPORTS NEWS BLOG | TANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA GHARAMA NAFUU KWA MAELEZO ZAIDI WASILIANA NASI: 0654315901 | Barua Pepe: urary95@yahoo.com
 
Back to top!