Searching...
Friday, July 23, 2010

Wanajeshi wa Uganda wauawa Somalia

Baadhi ya askari wa kulinda amani Somalia

Baadhi ya askari wa kulinda amani Somalia

Wanajeshi wawili kutoka Uganda wanaolinda amani nchini Somalia chini ya Muungano wa Afrika wameuawa mjini Mogadishu.

Askari hao waliuawa katika mapigano kati ya vikosi vya AU na wapiganaji wa kiislam wa al-Shabaab.

Msemaji wa Muungano huo amethibitisha kujeruhiwa kwa wanajeshi wengine watatu.

Kwa mjibu wa jeshi la Muungano wa Afrika majeshi yamelazimika kuondoka katika ngome yake katika mji wa Mogadishu na kuelekea vitongojini ili kuwasaka wapiganaji hao.

Suala la hali ya usalama nchini Somalia huenda likawa ajenda kuu katika kikao cha viongozi wa nchi na serikali wa Muungano wa Afrika kitakachoanza mjini Kampala, Uganda wikendi hii

Habari na Bbcswahili

0 comments:

WELCOME URARY95 SPORTS NEWS BLOG | ADVERTISE YOUR BUSINESS HERE AT A CHEAP PRICE MORE INFORMATION CONTACT US: 0654315901 | Email: urary95@yahoo.com | KARIBU URARY95 SPORTS NEWS BLOG | TANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA GHARAMA NAFUU KWA MAELEZO ZAIDI WASILIANA NASI: 0654315901 | Barua Pepe: urary95@yahoo.com
 
Back to top!