Searching...
Tuesday, July 27, 2010

'Polisi wauaji' mahakamani Misri

Kesi ya polisi wawili wa Misri wanaoshtakiwa kwa kufanya ukatili na kusababisha kifo cha mtu mwenye umri wa miaka 28 mwezi mmoja uliopota imeanza leo.

Khaled Said alikufa akiwa mikononi mwa polisi katika mtaa mmoja huko Alexandria mwezi Juni. Kesi hiyo imesababisha hasira kubwa nyumbani na nje.

Watetezi wa haki za binadamu wameandamana nje ya mahakama huku polisi wakiwa wameweka ulinzi mkali.

Maandamano Misri

Mashahidi wanasema Bw Said alifariki dunia baada ya kuburutwa kutoka kwenye mgahawa na kupigwa. Serikali inasema alimeza paketi ya dawa za kulevya na kupaliwa.

Taarifa kutoka shirika la kimataifa la Amnesty lililotolewa Jumatatu ilielezea wasiwasi kuwa mashahidi katika kesi hiyo wanaweza kuteswa na kuisihi serikali iwahakikishie usalama.

Marekani, Umoja wa Ulaya na makundi mengine ya kutetea haki za binadamu yote yametoa wito wa kufanywa uchunguzi wa wazi.

Habari na Bbcswahili

0 comments:

WELCOME URARY95 SPORTS NEWS BLOG | ADVERTISE YOUR BUSINESS HERE AT A CHEAP PRICE MORE INFORMATION CONTACT US: 0654315901 | Email: urary95@yahoo.com | KARIBU URARY95 SPORTS NEWS BLOG | TANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA GHARAMA NAFUU KWA MAELEZO ZAIDI WASILIANA NASI: 0654315901 | Barua Pepe: urary95@yahoo.com
 
Back to top!