Searching...
Monday, July 26, 2010

Kipindupindu yaripuka Cameroon, watu 77 wafariki dunia

Sample ImageWizara ya Afya ya Cameroon imetangaza kuwa takriban watu 77 wamefariki dunia kufuatia mripuka wa maradhi ya kipindupindu nchini humo. Taarifa ya wizara hiyo imesema kuwa kesi ya kwanza ya ugonjwa huo iliripotiwa mwezi Juni huku ikitahadharisha kuwa pana uwezekano mkubwa wa ugonjwa huo kusambaa katika nchi jirani za Chad na Nigeria.
Waziri wa Afya wa Cameroon Mama Fouda amewataka wananchi katika eneo hilo la kati mwa Afrika wawe waangalifu na kuripoti kesi zozote za kipindupindu mara moja. Nchi za kati mwa Afrika kwa kawaida hukumbwa na magonjwa kama hayo kutokana na umasikini mkubwa ulioko katika nchi za eneo hilo. Kwa mujibu wa Umoja wa Mataifa nchi nyingi za katikati mwa Afrika zinaongoza kwa umasikini barani Afrika zikilinganishwa na nchi za maeneo mengine ya bara hilo.

0 comments:

WELCOME URARY95 SPORTS NEWS BLOG | ADVERTISE YOUR BUSINESS HERE AT A CHEAP PRICE MORE INFORMATION CONTACT US: 0654315901 | Email: urary95@yahoo.com | KARIBU URARY95 SPORTS NEWS BLOG | TANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA GHARAMA NAFUU KWA MAELEZO ZAIDI WASILIANA NASI: 0654315901 | Barua Pepe: urary95@yahoo.com
 
Back to top!