Searching...
Sunday, June 20, 2010

Zimbabwe waongoza kwa kuomba hifadhi nje

watoto wa zimbabwe

Watoto wakiokota mahindi yaliyomwagika barabarani wakati wa kusafirishwa kutoka Afrika Kusini kuingia Zimbabwe mwaka jana.

"Wazimbabwe 158,000 waliomba hifadhi nje ya nchi mwaka jana"

Idara ya wakimbizi ya Umoja wa Mataifa - UNHCR - inasema Wazimbabwe wanaongoza duniani katika kuomba hifadhi ya kisiasa katika nchi za nje.

UNHCR inasema Wazimbabwe 158,000 wameomba hifadhi katika nchi za nje mwaka jana, wengi wao katika nchi jirani, Afrika Kusini.

Ripoti hiyo inasema watu kutoka Burma wanashika nafasi ya pili kwa kuomba hifadhi nje. Nchi nyingine ambazo zinatoa waombaji hifadhi nje kwa wingi ni pamoja na Afghanistan, Colombia, Eritrea, Ethiopia na Somalia.

Makadirio yanaonyesha kuwa Wazimbabwe wapatao millioni tatu wamekimbilia Afrika Kusini katika kipindi cha miaka kumi iliyopita kuepuka machafuko ya kisiasa na kutokana na kuanguka kwa uchumi Zimbabwe.

0 comments:

WELCOME URARY95 SPORTS NEWS BLOG | ADVERTISE YOUR BUSINESS HERE AT A CHEAP PRICE MORE INFORMATION CONTACT US: 0654315901 | Email: urary95@yahoo.com | KARIBU URARY95 SPORTS NEWS BLOG | TANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA GHARAMA NAFUU KWA MAELEZO ZAIDI WASILIANA NASI: 0654315901 | Barua Pepe: urary95@yahoo.com
 
Back to top!