MSHAMBULIAJI
wa Atletico Madrid, Diego Costa anaweza kuwa katika jaribio la kuing'oa
Chelsea katika Ligi ya Mabingwa Ulaya, lakini alikuwa mwenye furaha
kupita kiasi wakati anawapungia mkono mashabiki wa timu hiyo baada ya
mechi ya jana.
Inafahamika
mshambuliaji huyo ni chaguo la kwanza la kocha Jose Mourinho katika
orodha ya wachezaji anaotaka kuwasajili msimu ujao na kitendo cha
kuwapungia kwa furaha mashabiki wa Chelsea jana kimezidi kuongeza dalili
za kuhamia kwake London.
Chelsea
ilitoka sare ya bila kufungana na Atletico Madrid Uwanja wa Vicente
Calderon, inamaanisha mchezo bado upo kati kwa kati kuelekea mechi ya
marudiano Jumatano ijayo.
Upinzani: Mshambuliaji huyo anaweza kuja kuwa mchezaji mwenzake John Terry msimu ujao, japokuwa jana walizinguana sana uwanjani
Baada ya filimbi ya mwisho mashabiki wa Chelsea walibaki uwanjani wakati baadhi ya wachezaji wanapita mbele yao kuondoka.
Na wakati Costa alipofika kwenye eneo lao, mashabiki wa Chelsea wakaanza kuimba: "Diego Costa, tutakuona mwaka ujao,".
Mshambuliaji
huyo wa Atletico aliwapigia makofi pia na kuufurahia wimbo huo. Wakati
ukifika utatoa majibu katika kipindi cha pili cha Mourinho kuiongoza The
Blues na hata kuhusu mustakabali wa mchezaji ghali wa klabu hiyo,
Fernando Torres kama rekodi yake itavunjwa?
0 comments:
Post a Comment