Searching...
Thursday, July 19, 2012

Idadi ya waliofariki Zanzibar yazidi 30


Miili ya watu walioangamia baada ya feriu kuzama Zanzibar
Miili ya watu walioangamia baada ya feriu kuzama Zanzibar
Takriban watu 30 wamefariki dunia baada ya meli iliyokuwa imewabeba abiria zaidi ya mia mbili na hamsini kuzama karibu karibu na kisiwa cha Zanzibar nchini Tanzania .
Kwa mujibu wa taarifa zilizitolewa na kikosi cha wanamaji, watu wengine wengi wanaripotiwa kuokolewa kufuatia meli hiyo kuzama kutokana na dhoruba kali.
Mmoja wa watu waliofika katika eneo kulikotokea ajali hiyo na kushiriki katiia uokoaji ni Mohammed Omar ambaye aliambia BBC kuwa meli hiyo ilikuwa imepinduka na injini zake zikiwa juu: "wengi wa waliookoka ni wale wanaojua kuogolea vivi hivi na Mwenyezi Mungu."
Mwandishi wetu wa Dar Es Salaam, Hassan Mhelela, ambaye amekuwa akifuatilia ajali hiyo tangu itokee jana amesema shughuli za uokoaji zimeripotiwa kuanza tena.
Alisema zilisimamishwa jana usiku kwa sababu ya hali mbaya ya bahari na giza.
Mwaka mmoja haujakamilika tangu kutokea ajali nyingine kutoka katika njia hiyohiyo ya meli na kusababisha vifo vya mamia ya watu.
Kwa hisani ya bbcswahili

0 comments:

WELCOME URARY95 SPORTS NEWS BLOG | ADVERTISE YOUR BUSINESS HERE AT A CHEAP PRICE MORE INFORMATION CONTACT US: 0654315901 | Email: urary95@yahoo.com | KARIBU URARY95 SPORTS NEWS BLOG | TANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA GHARAMA NAFUU KWA MAELEZO ZAIDI WASILIANA NASI: 0654315901 | Barua Pepe: urary95@yahoo.com
 
Back to top!